National Water Board Chairman at Ministry of Water

Vacancy title:
National Water Board Chairman

[ Type: FULL TIME , Industry: Utilities , Category: Admin & Office ]

Jobs at:

Ministry of Water

Deadline of this Job:
15 October 2021  

Duty Station:
Within Tanzania , Dodoma , East Africa

Summary
Date Posted: Monday, September 20, 2021 , Base Salary: Not Disclosed


JOB DETAILS:
Nafasi Ya Mwenyekiti Wa Bodi Ya Maji Ya Taifa
Katibu Mkuu, Wizara ya Maji anatangaza nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Maji ya Taifa. Bodi hii inaundwa kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na. 11 ya mwaka 2009 chini ya Kifungu Na. 20. Muda wa Bodi ni miaka mitatu.

Majukumu Ya Bodi Ya Maji Ya Taifa
(a) Kuchunguza jambo lolote litakalowasilishwa kwake na Waziri au Wizara ya Sekta nyingine kuhusiana na usimamizi endelevu wa rasilimali za maji na kutoa mapendekezo yao kwa Waziri au Wizara ya Sekta husika, itakavyoona inafaa, kuchukua hatua madhubuti ili kufikia malengo ya Sheria hii:
(b) Kushauri vipaumbele vya uwekezaji na mpangilio wa kifedha na kuratibu na kuunganisha miradi inayotekelezwa kwa fedha za nje na programu zenye kutoa mchango wa kuendeleza rasilimali za maji:
(c) kushauri katika kujumuisha mipango ya sekta mbalimbali kuhusu tathmini na kupanga rasilimali za maji:
(d) kushauri uratibu wa mipango ya bonde na usimamizi
(e) kushauri utatuzi wa migogoro kati ya sekta moja na nyingine na kati ya Bonde moja na lingine
(f) kushauri vipaumbele vya uwekezaji na mpangilio wa kifedha,
(g) kushauri uhamisho wa maji baina ya mabonde:
(h) Kushauri usimamizi wa rasilimali za maji shirikishi.
(i) kupendekeza kwa Waziri hatua za kisheria kwa ajili ya usimamizi wa rasilimali za maji na njia madhubuti ya kuzuia uchafuzi wa maji:
(j) Kushirikiana na Mkurugenzi kwenye masuala ya kiufundi
(k) Kuandaa taarifa ya kila nusu mwaka ya hali ya rasilimali za maji: na
(l) Kutekeleza majukumu mengine ya kiushauri ya Sekta kama Waziri atakavyoona inafaa.

Sifa Za Mwombaji
Mwombaji wa nafasi hii anatakiwa kuwa na ujuzi na uzoefu katika masuala ya Sekta ya Maji au Sekta zinazohusiana na sekta hiyo. Awe na uzoefu na ujuzi katika masuala ya uongozi na usimamizi katika nyanja zinazohusiana na masuala ya usimamizi wa rasilimali za maji kwa muda usiopungua miaka 10. Aidha, awe na ujuzi mahsusi kwenye masuala ya usimamizi wa rasilimali za maji na asiwe/ asitoke kwenye taasisi ambayo ni mtumiaji mkuu wa maji (Major Water User).

Education Requirement: No Requirements

Work Hours: 8


Experience in Months: 120

 

{module 312}

Job application procedure
Maombi yatumwe kwa:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Maji,
Mji wa Serikali,
Mtaa wa Maji,
S.L.P. 456,
40473, Dodoma
Nakala ya maombi itumwe kupitia barua pepe: ps@maji.go.tz

Maombi yaambatishwe na wasifu wa mwombaji (CV) yenye wadhamini watatu na namba zao za simu. Andika "Mwenyekiti Bodi ya Maji ya Taifa" nyuma ya bahasha.
Mwisho wa kupokea maombi ni siku ya Ijumaa tarehe 15 Oktoba, 2021 saa 09.30 alasiri


All Jobs

QUICK ALERT SUBSCRIPTION

{module 316}

Job Info
Job Category: Administrative jobs in Tanzania
Job Type: Full-time
Deadline of this Job: 15 October 2021
Duty Station: Dodoma
Posted: 20-09-2021
No of Jobs: 1
Start Publishing: 20-09-2021
Stop Publishing (Put date of 2030): 20-09-2065
Apply Now
Notification Board

Join a Focused Community on job search to uncover both advertised and non-advertised jobs that you may not be aware of. A jobs WhatsApp Group Community can ensure that you know the opportunities happening around you and a jobs Facebook Group Community provides an opportunity to discuss with employers who need to fill urgent position. Click the links to join. You can view previously sent Email Alerts here incase you missed them and Subscribe so that you never miss out.

Caution: Never Pay Money in a Recruitment Process.

Some smart scams can trick you into paying for Psychometric Tests.